Chelsea wamekubali kumsajili winga wa Sporting Geovany Quenda.Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka saba Stamford Bridge na chaguo la msimu wa ujao baada ya ada ya takriban £40m kukubaliwa.
Chelsea ina machaguo mengi kwa pande zote mbili lakini wanaamini kuwa Quenda, ambaye hatajiunga na klabu hiyo hadi 2026, ana uwezo wa kucheza kila upande na anaweza kuwashinda mabeki kwa pambano la moja kwa moja.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno chini ya umri wa miaka 21 amefunga mabao mawili na ametoa pasi nane za mabao katika mechi 43 tangu aingie kwenye kikosi cha kwanza cha Sporting.
Kinda huyo alikuwa akihusishwa na kuhamia Manchester United ili kuungana na meneja wake wa zamani Ruben Amorim.

0 Comments