SIMBA WAMKUMBUKA BABRA GONZALES KISA HERSI

 Anaandika mdau love sport star

𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐁𝐀 𝐖𝐀𝐉𝐔𝐓𝐈𝐄 𝐊𝐔𝐌𝐔𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐁𝐀𝐁𝐑𝐀 



Kosa kubwa walilolifanya Simba ni Kumdondosha Bavbra Gonzalez Kipindi ambacho alikuwa kwenye Peak ya mafanikio Ndani na nje ya Africa.

Walafi wa Madaraka walimzima Bavbra Kama Mshumaa wa birthday.

Kutoka Kuzungumzwa Africa, Kuhudhuria Vikao vya CAF hadi Kuwa mjumbe wa CAF alishafanikiwa Kuibrand Simba 100%

Walikuja wakamzima Bavbra bila kujua Wanaizima brand ya Simba.

Tazama Leo mtoto wa Mzee Ally wa kinondoni Engeneer Hersi Aliamu kupita njia zile zile za Bavbra Gonzalez, Alichokifanya ni Kuongeza bidii kufika Mbali zaidi ya Pale alipokuwa Bavbra.Leo Engeneer Hersi Saidi hazungumzwi tu CAF hadi FIFA Wamemuamini sasa ni Mjumbe wa mashindano ya Vilabu Duniani 

Kumbuka Alipokuwa Bavbra alikuwa anaenda kwa jina la Simba,Leo Engeneer Hersi Saidi Anaenda kwa jina la Yanga..

Kiongozi Bora huifanya brand Kubwa Bora.

Ukaribu wa Engeneer Hersi na Infantino unaleta Matunda.Sasa Anaweza kuaminiwa TFF,CECAFA na CAF, Infantino akiweka mkono wake Huyu anapita kuwa kiongozi.

Ana mabaya yake Mengi kuihusu Simba kama hasimu lakini mazuri pia anayo.No one always is Perfect.

Bibilia Inasema Mwanamke mpumbavu Huiharibu Nyumba yake Kwa Mikono yake Mwenyewe.Neno hili nalifananisha na Uongozi wa Simba hasa wale walisimama kidete kuzima Ndoto za Bavbra Gonzalez bila Kujua wanaharibu future ya mafanikio ya Club.Kama Bavbra angeachwa unazani hizi Nafasi anazopata Engeneer Hersi angezipata Mbele ya Bavbra Gonzalez???

Wanasimba Tunaweza tukasema hakuna jipya analolifanya Engeneer Hersi kwasababu yalifanywa na Bavbra, lakini Kumbukumbu Bavbra alifanya akaishia njiani, Engeneer kafanya Zaidi ya Bavbra Gonzalez no matter utamchukia but this is reality.Leo FIFA wanamwamini Yeye kama icon!

Time is now: Ukisahau ulipotoka Utapotea unakokwenda.Viongozi wasipojitafakari mapungufu Simba itapotea Zaidi ya Hapo



Post a Comment

0 Comments