TETESI ZA USAJILI DUNIANI JANUARI 20,2025

 Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Ibrahima Konate, 26, yuko katika msimu wake wa tano Anfield na anaamini anastahili kuwa mmoja wa mabeki wanaolipwa vizuri zaidi kwenye Ligi ya Premia. (Team talk)

Liverpool inaweza kumsajili beki wa Tottenham Micky van de Ven, kuchukua nafasi ya Konate na huku Real Madrid ikizingatia mustakabali wa beki huyo wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 24. (Team Talk)

Manchester United inamfuatilia kiungo wa kati wa Sunderland Noah Sadiki, 21, na inaweza kumtoa kiungo wa kati wa Uruguay Manuel Ugarte, 24, katika mkataba wa kubadilishana na mchezaji huyo wa kimataifa wa DR Congo. (Give me Sport)


Kobbie Mainoo anatarajiwa kusalia Manchester United kufuatia uteuzi wa kocha wa muda Michael Carrick. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20, ambaye ameichezea England mechi 10, alikuwa akifikiria kuhama kwa mkopo ili kupata muda wa kucheza. (Fabrizio Romano)

Post a Comment

0 Comments