Vilabu kadhaa vya Ligi Kuu England vimefunguliwa milango ya matumaini ya kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ufaransa Eduardo Camavinga, 23, baada ya Real Madrid kuwa tayari kusikiliza ofa kwa ajili yake dirisha la majira ya kiangazi. (Marca)
Arsenal wameanza mazungumzo na RB Leipzig kuhusu kumsajili beki wa kati wa Ufaransa Castello Lukeba, 23. (L'Equipe)
Chelsea, Liverpool na Manchester United zinatarajiwa kupambana kusaka saini ya kiungo wa Crystal Palace na England Adam Wharton, 22. (Football Insider)
Chelsea na Manchester United pia zinatajwa kuwa katika ushindani mwingine wa uhamisho, huku zote zikiwa miongoni mwa vilabu vinavyomtaka mshambuliaji wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 19 Said El Mala kutoka 1. FC Köln. (Caughtoffside)
Mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 28, anaweza kurudi Manchester United baada ya muda wake wa mkopo Barcelona, ambao wanamtaka winga wa Chelsea na Ureno Pedro Neto, 26, kama mbadala. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Rashford anataka kubaki Barca, lakini mazungumzo yamegonga mwamba na mkurugenzi wa michezo Deco amependekeza msimu mwingine wa mkopo ili kuwapa timu hiyo ya Uhispania muda zaidi wa kulipa ada ya chaguo la kumnunua kutoka kwa Manchester United. (Talksport)

Tottenham wanaandaa chaguzi zinazowezekana za kuchukua nafasi ya Igor Tudor kama kocha mkuu ikiwa wataamua kufanya mabadiliko mengine ya usimamizi. (Athletic - subscription required)

0 Comments