PSG YAIBAGAZA ARSENAL ,VITINHA AWA GUMZO

 Dakika 90 na zile 30 za nyongeza za mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Arsenal na PSG zilikamilika huku timu zote mbili zikiwa sare ya 1-1. Mikwaju ya penati ikaamua mshindi PSG ikipata penati 4- 3.


Arsenal walitangulia kwa bao la mapema lililofungwa na Kai Havertz katika dakika ya 6, kabla ya PSG kusawazisha kupitia penalti ya Ousmane Dembélé katika dakika ya 65.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani mkali, Arsenal wakionekana kuwa na nidhamu nzuri ya ulinzi huku PSG wakitawala zaidi umiliki wa mpira na kujaribu kutengeneza nafasi.

PSG inakuwa timu ya pili kuandika historia katika muongo uliopita kwa kuweza kutetea taji hilo, ililolitwaa msimu uliopita kwa kuchapa Inter Milan 5-0, ikifuata nyayo za Real Madrid

 Vitinha awa gumzo 

Kiungo Vitinha aliibuka nyota wa mchezo huo akiisaidia PSG kumiliki mpira kwa dakika zote 106, Wataalamu wa lugha wamempachika nyota huyo jina la injini ya PSG kutokana na ubora aliokuwa nao.
Nyota huyo mwenye miaka 26 alikokota mipira mara 162 na kupiga jumla ya pasi fupi 141 pasi ndefu 4, mashuti yaliyoelekea langoni 4 na kunyang'anya mipira mara 5. 
Nyota huyo aliifanya Arsenal ishindwe kucheza vyema hasa eneo la katikati lililokuwa linaundwa na Declan Rice pamoja na Myles Lewis Skelly


LUIS ENRIQUE AFIKIA REKODI ZA GUARDIOLA,ZIDANE UEFA 

Kocha wa PSG luis Enrique ameendelea kuandika historia katika michuano ya Ulaya baada ya kufanikiwa kutwaa makombe matatu ya UEFA, Kocha huyo alifanikiwa kutwaa ubingwa wake wa kwanza wa UEFA akiwa Barcelona msimu wa 2014/15 baada ya kuifunga Juventus mabao 3-1 
Msimu wa 2024/25 alitwaa taji la pili akiifunga Inter Milan kwa mabao 5-0 na msimu huu ameifunga Arsenal kwa mikwaju ya penati 4-3

Kocha huyo amezifikia rekodi za Pep Guardiola aliyeisaidia Barcelona kutwaa taji la UEFA msimu wa 2009 na 2011 akiifunga Manchester United kisha kutwaa taji la tatu akiwa na Manchester City baada ya kuifunga Inter Milan bao 1-0.
Licha ya kutwaa ubingwa huo mara tatu bado hajafikia rekodi za Zinedine Zidane aliyetwaa ubingwa wa UEFA mara tatu mfululizo akizifunga Atletico Madrid 5-3 kwa mickwaju ya penati baada ya dakika 120 kwa sare ya 1-1 msimu wa 2015/16. Msimu wa 2016/17 waliingia tena fainali na kuifunga Juventus 4-1 na msimu wa 2017/18 alitwaa tena ubingwa huo kwa kuifunga Atletico Madrid mabao 4-1.
Kocha Carlo Ancelotti anasalia kinara wa kom,be hilo akitwaa mara mara 5 akiwa na AC Milan vikombe viwili mwaka 2002/2003 na 2006/2007 .Real Madrid mwaka 2014,2022 na 2024

Post a Comment

0 Comments