''Hongereni Simba Queens kwa kutwaa ubingwa wa ligi kwa mara nyingine tena. Kwa mafanikio ya mataji matano ya ligi na kufika hatua ya nusu fainali ya CAF Women’s Champions League, Simba Queens imeendelea kujidhihirisha kama moja ya timu zilizoweka alama kubwa zaidi katika soka la wanawake nchini Tanzania.
Mafanikio haya yanatupa sababu ya kujivunia, lakini bado tuna malengo makubwa zaidi.Lengo letu ni kuona Simba Queens ikitwaa ubingwa wa CAF Women’s Champions League na kuipeperusha bendera ya Tanzania barani Afrika.Hongereni Simba Queens. Safari bado inaendelea''
Naye mlezi wa klabu hiyo Fatema Dewji aliwakabidhi wachezaji hao kiasi cha shilingi milioni 10 kama pongezi kwa uwezo mzuri waliouonyesha msimu huu na kunukuliwa akisema
''Asante kwa kila mchezaji, benchi la ufundi, viongozi, mashabiki na wadau wote walioamini safari hii. Huu ni mwanzo wa mafanikio makubwa zaidi kwa Simba Queens…tukiwa mabingwa wa Tanzania, sasa macho yetu yanaelekezwa kwenye ushindani wa kimataifa na kuendelea kuipeperusha bendera ya Simba na Tanzania kwa ujumla

0 Comments